Nenda kwa yaliyomo

Madagaska

Majiranukta: 20°S 47°E / 20°S 47°E / -20; 47
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Madagascar)
Jamhuri ya Madagaska
Repoblikan’i Madagasikara (Malagasy)
République de Madagascar (French)
Kaulimbiu: Fitiavana, Tanindrazana, Fandrosoana
(Love, Fatherland, Progress)
Wimbo wa taifa: Ry Tanindrazanay malala ô!
Mahali pa Madagaska
Mji mkuu
na mkubwa
Antananarivo
Lugha rasmiMalagasy, French
Kabila (2017)
  • Wamerina
  • Wabetsimisaraka
  • Wabetsileo
  • Watsimihety
  • Wasakalava
  • Waantaisaka
  • Waantandroy
  • Makabila Mengine
 • Rais
Andry Rajoelina
 • Waziri Mkuu
Christian Ntsay
Historia
 • Ufalme wa Madagascar
Karne ya 16
 • Koloni la Kifaransa
6 Agosti 1896
 • Uhuru kutoka Ufaransa
26 Juni 1960
Eneo
 • Jumlakm2 592,796 km² (ya 46)
 • Maji (asilimia)0.9%
Idadi ya watu
 • Kadirio la 202431,964,956
 • Msongamano55/km²/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2023
 • Jumla $56.754 bilioni
 • Kwa kila mtu $1,906
PLT (Kawaida)Kadirio la 2023
 • Jumla $15.763 bilioni
 • Kwa kila mtu $529
HDI (2022) 0.487
Gini (2012)decrease 42.6
SarafuAriary (MGA)
Majira ya saaUTC+3 (EAT)
Msimbo wa simu+261
Jina la kikoa.mg
Ramani ya Madagaska.

Madagaska, rasmi Jamhuri ya Madagaska ni nchi ya kisiwa iliyoko katika Bahari ya Hindi, takriban kilomita 400 (maili 250) kutoka pwani ya kusini-mashariki mwa Afrika. Ni kisiwa cha nne kwa ukubwa duniani, kikiwa na eneo la kilomita za mraba 592,796 (maili za mraba 228,880). Nchi hii inajulikana kwa viumbe hai wake wa kipekee, ambapo zaidi ya 90% ya wanyama na mimea yake hupatikana tu huko. Madagaska ina mifumo mbalimbali ya ikolojia, ikiwa ni pamoja na misitu ya mvua, misitu mikavu ya majani yanayopukutika, na maeneo ya miiba, na kuifanya kuwa moja ya maeneo muhimu zaidi ya viumbe hai duniani. Mji mkuu na mkubwa zaidi, Antananarivo, ni kitovu cha kisiasa, kiuchumi, na kitamaduni cha nchi.

Kisiwa hiki kilianza kuwa na watu wanaozungumza lugha za Kiaustronesia karibu mwaka 500 BK, na baadaye kulifuata uhamiaji kutoka Afrika, Mashariki ya Kati, na Ulaya. Madagaska baadaye ilikuwa Ufalme wa Imerina kabla ya kutawaliwa na Ufaransa mnamo 1896. Nchi ilipata uhuru wake kutoka kwa Ufaransa tarehe 26 Juni 1960, na sasa ni jamhuri ya umoja yenye mfumo wa nusu-urais. Lugha rasmi ni Kimalagasi na Kifaransa, na idadi kubwa ya watu wanafuata Ukristo, mara nyingi ukiwa umechanganyika na imani za jadi. Uchumi wa Madagaska unategemea sana kilimo, uchimbaji madini, na utalii, huku vanilla na karafuu zikiwa miongoni mwa mazao yanayouzwa nje. Hata hivyo, nchi inakabiliwa na changamoto kama vile ukosefu wa utulivu wa kisiasa, umaskini, na uharibifu wa mazingira.

Jina Madagaska lina maana ya "Kisiwa kikubwa" na linatokana na lugha ya wenyeji, Wamalagasi ambao waongea Kimalagasi.

Jiografia

[hariri | hariri chanzo]

Kisiwa chenyewe ni cha nne kwa ukubwa duniani.

Upekee wa kisiwa unatokana na kwamba kilimeguka kutoka India miaka milioni 88 hivi iliyopita, halafu kilibaki bila watu hadi karne ya 5 hivi BK.

Ekolojia

[hariri | hariri chanzo]

Kisiwa hicho ni pia mazingira makubwa ya aina ya violezo ambayo ni asilimia 5 ya violezo vyote vya mimea na wanyama vya dunia nzima.

Asilimia 90 ya viumbehai asili ni maalumu wa Madagaska, kama vile wanyama aina ya kima awali wanaoitwa lemuri, ndege ambao waambukiza ugonjwa na mti wa mbuyu.

Historia

[hariri | hariri chanzo]
Mfalme Andrianampoinimerina (1787-1810).
Bendera ya Ufalme wa Merina.
Nembo ya Ufalme wa Merina.

Madagaska ni kati ya maeneo ya mwisho kufikiwa na kukaliwa na binadamu.

Wa kwanza kufika walitokea visiwa vya Indonesia (kama mwaka 350-550 BK).

Baadaye tu walihamia watu kutoka bara la Afrika (mwaka 1000 hivi) na wengineo (Waarabu, Wahindi, Wazungu, Wachina n.k.).

Kuanzia mwaka 1787 hadi mwaka 1897 kisiwa kilizidi kuunganishwa kisiasa chini ya Ufalme wa Merina.

Watawala walikuwa watu kutoka familia ya Andrianampoinimerina, mwanzilishi wa taifa hilo, ambaye alikuwa ametokea katika kabila la Wamerina

Kabila hilo lilikuwa kubwa na muhimu kuliko yote 18 ya kisiwa hicho. Makazi yake yalikuwa katika uwanda wa juu wa kati lakini lilienea sehemu kubwa ya Bukini.

Wamerina walikuwa na makao makuu ya utawala wao Antananarivo; baada ya kugawiwa kwa ufalme wao mnamo 1710 kitovu cha malaka kati ya Wamerina ikahamia kwenye mlima wa Ambohimanga lakini tangu kuunganishwa kwa Wamerina mnamo 1794 mji mkuu ukulikuwa tena Atananarivo. Kutoka hapo waliweza kueneza mamlaka yao katika sehemu nyingine za kisiwa hicho.

Makabila yote ya wenyeji yalizungumza lugha moja na yalikuwa na mila na desturi zinazofanana, hivyo yaliweza kujenga umoja wa kiutamaduni uliowafanya wawe jamii moja kimsingi.

Watawala hao wa kifalme waliweza kutekeleza mambo mbalimbali kuendeleza Bukini katika vipindi vyao kabla ya kuja kwa wageni kutoka Uingereza na Ufaransa ambao kwa kiasi fulani ulidhoofisha mamlaka ya kifalme.

Kisiwa hicho hatimaye kiligeuzwa kuwa koloni la Ufaransa. Hii ni kwa kuwa, ingawa sera ya kuisasisha ya Bukini kwa namna fulani iliimarisha uwezo wa nchi hiyo wa kutetea uhuru wake, lakini kwa ujumla sera hiyo ilidhoofisha ufalme huo kwa kuongeza utegemezi wake kwa mataifa ya kigeni.

Demografia

[hariri | hariri chanzo]
Mtoto wa Kimalagasi anayeonyesha kuwa na mchanganyiko wa damu.

Mwaka 2018 idadi ya wakazi ilikadiriwa kuwa milioni 26.3. Wenyeji wengi wana mchanganyiko wa damu: DNA inaonyesha kuwa wakazi wa kwanza kutoka Indonesia wameichangia asilimia 50 hivi na Waafrika vilevile. Wanaoishi sehemu za ndani ni wa Kiindonesia zaidi, wakati wale wa pwani ni wa Kiafrika zaidi.

Lugha ya taifa ni Kimalagasi. Lugha rasmi za Madagaska ni Kimalagasi na Kifaransa (angalia pia orodha ya lugha za Madagaska).

Mwaka 1993 nchini Madagaska kulikuwa na dini za jadi (52% hivi), Ukristo (41%, Waprotestanti wakiwazidi kidogo Wakatoliki), Uislamu (7% hivi) n.k. Tangu hapo wafuasi wengi wa dini za jadi wameongokea Ukristo, hasa wa Kiprotestanti.

Utamaduni

[hariri | hariri chanzo]

Pamoja na kutokea mazingira tofauti sana, Wamalagasi wamechanganyikana sana na kuwa na utamaduni na lugha aina moja, ya Kiindonesia zaidi.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

20°S 47°E / 20°S 47°E / -20; 47

Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Madagaska kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.