Nenda kwa yaliyomo

Timotheo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Timotheo, mmoja kati ya maaskofu wa kwanza, alivyochorwa katika Nuremberg chronicles f 109v(1493).
Picha takatifu ya Kiorthodoksi.

Timotheo (labda Listra, 17 hivi - Efeso, 97) ni mfuasi mpendwa wa Mtume Paulo, halafu mwandamizi wake [1].

Paulo alimuandikia barua mbili zilizopokewa katika Biblia kati ya Nyaraka za Kichungaji. Habari zake tunazipata humo na katika Matendo ya Mitume.

Tangu kale anaheshimiwa kama askofu mtakatifu na Wakatoliki na Waorthodoksi.

Tangu mwaka 1969, Kanisa Katoliki la Kilatini linamwadhimisha pamoja na Tito tarehe 26 Januari, siku inayofuata ile ya Uongofu wa Mt. Paulo, mwalimu wao.[2][3][4]. Waorthodoksi wanamuadhimisha tarehe 22 Januari.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Timotheo kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.