Zimbabwe
Jamhuri ya Zimbabwe Republic of Zimbabwe | |
---|---|
Kaulimbiu: "Unity, Freedom, Work" (Kiingereza kwa "Umoja, Uhuru, Kazi") | |
Wimbo wa taifa: "Blessed be the Land of Zimbabwe" | |
Mji mkuu na mkubwa | Harare |
Lugha rasmi | Kiingereza, Kishona, Sindebele |
Kabila (2023) | 99.4% Waafrika 0.2% Wazungu 0.4% Wengine |
Serikali | Jamhuri ya rais wa umoja |
• Rais | Emmerson Mnangagwa |
• Makamu wa Rais | Constantino Chiwenga |
Uhuru kutoka Uingereza | |
• Uhuru kutoka Uingereza | 18 Aprili 1980 |
• Tangazo la Jamhuri | 18 Aprili 1980 |
Eneo | |
• Jumla | km2 390,757 km² (ya 60) |
• Maji (asilimia) | 1% |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2024 | 16,868,409 |
• Msongamano | 39/km2 |
PLT (PPP) | Kadirio la 2023 |
• Jumla | ▲ $44.448 bilioni (ya 131) |
• Kwa kila mtu | ▲ $2,749(ya ) |
PLT (Kawaida) | Kadirio la 2023 |
• Jumla | ▲ $32.424 bilioni |
• Kwa kila mtu | ▲ $2,005 |
HDI (2022) | ![]() |
Gini (2019) | ▲ 50.3 |
Sarafu | Dola ya Zimbabwe (ZWL), Dola ya Marekani (USD) |
Majira ya saa | UTC+2 CAT |
Upande wa magari | Kushoto |
Msimbo wa simu | +263 |
Jina la kikoa | .zw |
Zimbabwe, rasmi kama Jamhuri ya Zimbabwe, ni nchi inayopatikana katika Afrika ya Kusini, bila pwani, inayopakana na Zambia kaskazini, Msumbiji mashariki, Afrika Kusini kusini, na Botswana magharibi. Ina idadi ya watu takriban milioni 16.7, ikiwa ya 73 duniani. Jiji lake kubwa zaidi na mji mkuu ni Harare. Zimbabwe imegawanyika katika majimbo 10. Inajulikana kwa historia yake ya ustaarabu wa kale, hasa mji wa mawe wa Zimbabwe Kuu, maporomoko maarufu ya Victoria Falls, na historia yake ya kisiasa, ikiwemo utawala wa muda mrefu wa Robert Mugabe na changamoto za kiuchumi zilizoshuhudiwa katika karne ya 21.
Jina
Jina Zimbabwe linatokana na neno "dzimba dzamabwe" linalomaanisha "nyumba ya mawe" kwa lugha ya Kishona. Nyumba hiyo ya mawe, ambayo imehifadhiwa kama eneo la kihistoria, ilikuwa makao ya Ufalme wa Mutapa ambaye mfalme wake aliongoza eneo hilo miaka ya kale.


Eneo
Zimbabwe imegawiwa katika mikoa 8 na miji 2 yenye hadhi ya mikoa. Imegawiwa zaidi katika wilaya 59 na kata 1,200.
- Bulawayo (mji),
- Harare (mji),
- Manicaland,
- Mashonaland ya Kati,
- Mashonaland Mashariki,
- Mashonaland Magharibi,
- Masvingo,
- Matabeleland Kaskazini,
- Matabeleland Kusini na
- Midlands.
Miji minne mikubwa ya Zimbabwe ni:
- Bulawayo, mji wa pili kwa ukubwa
- Harare, mji mkuu
- Chitungwiza
- Mutare


Historia
Historia ya awali
Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani.
Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi.
Tangu karne ya 11, Zimbabwe ya leo imekuwa na falme imara kwenye njia muhimu ya biashara, hasa ufalme wa Mutapa.
Ukoloni
Kampuni ya British South Africa ya Cecil Rhodes iliweka mipaka ya sasa katika miaka ya 1890.
Koloni la Uingereza lilianzishwa mwaka 1923 kwa jina la Southern Rhodesia.
Mwaka 1965, serikali ya walowezi Wazungu ilijitangazia uhuru kwa jina la Rhodesia tu.
Baada ya miaka 14 ya kutengwa kimataifa na kupigana na raia Waafrika katika miaka ya 1970, mapatano ya mwaka 1979 yalikubali wakazi wote wawe na haki ya kupiga kura na nchi ikawa huru kweli kwa jina la Zimbabwe mwaka 1980.
Baada ya uhuru
Rais Robert Mugabe alipata umaarufu katika siasa kama mpiganaji dhidi ya ukoloni lakini pia kama aina ya dikteta aliyerudisha nyuma uchumi wa nchi.
Baada ya yeye kulazimishwa na wanajeshi kujiuzulu, tarehe 24 Novemba 2017 Emmerson Mnangagwa amekuwa rais mpya wa Zimbabwe.
Demografia
Kabila
Wakazi wengi (82%) ni wa kabila la Washona, 14% ni Wandebele, 2% ni wa makabila mengine ya Kiafrika, 1% ni machotara, Wahindi, Wazungu n.k.
Lugha
Kwa sasa lugha rasmi ni 16. Lugha kubwa ni Kishona (70%) na Kindebele (20%). Kiingereza ni lugha ya kwanza ya chini ya asilimia 2.5% za wakazi.
Dini
Upande wa dini, 84.1% ni Wakristo (hasa Waanglikana, Wakatoliki 8%, Wasabato na Wamethodisti). Waliobaki ni wafuasi wa dini asilia za Kiafrika (4.5%), ni Waislamu (0.7%), au hawana dini (10.2%) .
Tazama pia
- Wilaya za Zimbabwe
- Kata za Zimbabwe
- Orodha ya miji ya Zimbabwe
- Mawasiliano Zimbabwe
- Utamaduni wa Zimbabwe
- Orodha ya lugha za Zimbabwe
- Muziki wa Zimbabwe
- Waandishi wa Zimbabwe
- Mambo ya kigeni Zimbabwe
- Orodha ya nchi kufuatana na wakazi
- Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu
- Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu
- Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa
- Demografia ya Afrika
Tanbihi
Viungo vya nje
Serikali
- [1] Ilihifadhiwa 16 Machi 2016 kwenye Wayback Machine. Tovuti rasmi ya Bunge la Zimbabwe
- [2] Ilihifadhiwa 24 Oktoba 2008 kwenye Wayback Machine. Tovuti rasmi ya serikalimirror site
Habari
- Ardhi na siasa Ilihifadhiwa 15 Mei 2006 kwenye Wayback Machine.-BBC usanifu wa utekelezaji wa arthi.
- [3] Zimbabwe destruction: (hadithi ya mtu mmoja)
- New Zimbabwe UK-Based independent daily newspaper
- AllAfrica.com - Zimbabwe news headline links
- IFEX - Zimbabwe Ilihifadhiwa 27 Juni 2006 kwenye Wayback Machine. press freedom violations
- The Sunday Mirror Ilihifadhiwa 15 Juni 2006 kwenye Wayback Machine. weekly newspaper
- Zimbabwe Independent weekly newspaper
- The Zimbabwean UK-based independent weekly newspaper (gazeti ya wiingereza)
- The Herald State-owned daily newspaper
- Zimbabwe Situation A comprehensive collection of news stories concerning Zimbabwe from different sources
- Haikona! Zimbabwe News Blog Ilihifadhiwa 17 Aprili 2006 kwenye Wayback Machine. Taarifa ya habari Zimbabwe
Wanamgambo
Maelekezo
- (Chuo kikuu cha kolombia - Zimbabwe maelekezo ya WWW-VL
- Open Directory Project - Zimbabwe maelekezo
- Stanford University - Afrika kusini mwa Sahara: Zimbabwe maelekezo
- Yahoo! - Zimbabwe Ilihifadhiwa 6 Januari 2009 kwenye Wayback Machine. maelekezo
Utalii
- Travel Overview of Zimbabwe Ilihifadhiwa 9 Julai 2006 kwenye Wayback Machine.
- Facts about Zimbabwe Ilihifadhiwa 27 Aprili 2006 kwenye Wayback Machine.
Nyingine
- Amnesty International (Zimbabwe) Ilihifadhiwa 16 Juni 2006 kwenye Wayback Machine.
- Dariro (makala ya kutafuta vifungu vya Zimbabwe) Ilihifadhiwa 21 Aprili 2006 kwenye Wayback Machine.
- itsbho.com Leading Zimbabwean entertainment website Ilihifadhiwa 29 Machi 2018 kwenye Wayback Machine.
- RSF report on Zimbabwe from 2003 Ilihifadhiwa 21 Aprili 2005 kwenye Wayback Machine.
- Writers of Zimbabwe – (makala ya muadishi kwa waandishi wa Zimbabwe)
- Zimbabwe Human Rights NGO Forum-(haki za kibinadamu)
- ZIMBABWE Ilihifadhiwa 10 Mei 2005 kwenye Wayback Machine. (viungo via taarifa)
- "Dead Capital" in Zimbabwe Ilihifadhiwa 13 Agosti 2006 kwenye Wayback Machine.
- 5 year archive of Zimbabwe news updated daily
- Zimbabwe Crisis Habari za kuazua zilizo chapishwa wakati wa kura mnamo 2000.
- ZimFest Miziki ya Zimbabwe kila mwaka, Marekani kaskazini.
- Zimbabweb Ilihifadhiwa 9 Januari 2014 kwenye Wayback Machine. lango la taarifa Zimbabwe
- zwnews Lango la habari Zimbabwe
- Economic Development Bulletin (Maelezo ya maedeleo ya uchumi) kupoteza haki ya mali Zimbabwe na udhoofu wa uchumi.
- Cato Journal Ilihifadhiwa 2 Januari 2011 kwenye Wayback Machine. Kifungu cha kuanguka kwa nchi ya Zimbabwe
- Center for Global Development Ilihifadhiwa 6 Aprili 2006 kwenye Wayback Machine. (senta ya maedeleo ya dunia) garama na mwanzo wa misukosuko Zimbabwe.
Nchi za Afrika | ![]() |
---|---|
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe | |
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Zimbabwe kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |